Saturday 25 August 2012

TAARIFA YA USAFIRI KWENDA M4C READING

 TAWI LA CHADEMA UK LINAPENDA  KUWATANGAZIWA WANACHAMA WAKE WOTE, WATANZANIA WOTE NA WAPENZI WA CHADEMA WAISHIO LONDON KUWA  WAWASILIANE NA CHRIS LUKOSI KWA TARATIBU ZA USAFIRI WA KWENDA READING KUHUDHULIA MKUTANO WA M4C.

MAGARI YATAONDOKA SAA NNE ASUBUHI

Mkutano utafanyika siku ya Tarehe 26/08/2012 kuanzia saa saba mchana mpaka saa kumi na mbili jioni, siku ya Bank Holiday. Risc Reading International Solidarity Centre, 35-39 London Street, Reading, RG1 4PS .
 
WASOMI WENGI NA WANAHARAKATI MBALI MBALI WATAONGEA SIKU HIYO,
SIKU YA MKUTANO TUTAANZISHA MFUKO WA KUFA NA KUZIKANA KWA AJILI YA WATANZANIA WOTE WAISHIO UK BILA KUBAGUA CHAMA CHAKO CUF,CCM,UDP,TLP WOTE MNAKARIBISHWA
 
Watanzania wote na wadau mbali mbali mnakaribishwa
 
SISI SOTE NI NDUGU, TATIZO NI CCM
 
 ni wakati wa kusimama na kusema tumechoka
 
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA HAWA WAFUATAO
MWENYEKITI: Chris Lukosi 07903828119
 
Au tutumie email kupitia chademauk@gmail.com
 
 
Peooooople's Power

Friday 24 August 2012

Dk. Slaa: CCM wana sababu za kikoloni

 
KATIBU Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ), Dk. Willibrod Slaa, amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kinachukiwa na wananchi kutokana na kuendelea kujitetea kwa kutumia sababu zilizotumiwa na wapigania uhuru wa Tanganyika kujikomboa katika mikono ya wakoloni.

Akizungumza katika mikutano ya hadhara kwenye vijiji mbalimbali vya kata za Ngerengere na Makambarai, Dk. Slaa alisema serikali ya CCM imeshindwa kutengeneza fursa ya wananchi kujiletea maendeleo yao licha ya kuwa katika nchi yenye rasilimali nyingi.

“Mwalimu Nyerere pamoja na wapigania uhuru wengine wa Tanganyika hawakumkataa mkoloni kwa sababu ya rangi, dini wala hali zao isipokuwa waliwakataa kwa vile walishindwa kuwaondolea watu umaskini, ujinga na maradhi ambayo yanaendelea kutuandama kila wakati,” alisema.

Alisema kuwa hayati Mwalimu Nyerere alifikia malengo kwa kuonesha njia ya kupita, hivyo waliomfuatia walikuwa na wajibu wa kuhakikisha njia hiyo inapitika lakini serikali ya CCM imeamua kuziba njia hiyo.

Huku akisoma takwimu za maendeleo katika Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki, linaloongozwa na Dk. Lucy Nkya (CCM), Dk. Slaa alisema kuwa hakuna sababu ya kuendelea kukivumilia chama hicho kwa sababu ya kufanana kwa rangi na badala yake wananchi wanapaswa kuchukua hatua ya kukipumzisha.

“Kila mmoja hapa amesikia takwimu nilizosoma, tena zinatokana na vitabu vya serikali yenu hii mliyoichagua na kuiweka madarakani, mlichagua rais wa CCM, mbunge wa CCM, Diwani wa CCM, mwenyekiti wa kijiji na serikali ya kijiji ya CCM, sasa nawasomea hapa ufisadi unaofaywa mnaanza kusikitika,” alisema.

Alisema ni aibu miaka 50 baada ya Uhuru kusikia Watanzania wakizungumzia upungufu wa madawati wakati nchi nyingine zikiwa zinashindana kwenda kuangalia uwezekano wa kufanya utafiti utakaozisaidia nchi zao.


Taarifa Fupi kuhusu Kazi za Maendeleo Jimboni Ubungo (AMUA)

MR TWO "SUGU" AWASILI HOUSTON, MAREKANI TAYARI KWA KUWASHA MOTO JUMAMOSI 25 AUG 2012


Thursday 23 August 2012

Mwalimu mmoja wanafunzi 652

Akiwa katika Oparation Sangara inayoendelea hivi sasa nchini, Mwenyekiti wa Baraza la vijana la Chadema, Bwana Deogratias Munishi amegundua shule ambayo inawanafunzi 652 na Mwalimu mmoja tu. Shule hiyo ipo katika Kijiji cha Kadodo Kata ya  Luale, Mvomelo  Mkoani Morogoro.  Hii ndo hali halisi ya elimu Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru, chini ya utawala wa CCM. 
 
Mwenye shati la rangi ya udongo na suruali nyeusi ndiye Mwalimu Mkuu na Mwalimu pekee wa Shule ya Msingi Kododo iliyopo kata ya Luale, Mvomelo Mkoani Morogoro. Shule hiyo inawanafuzi 652.
 
 
Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi akiwasikiliza kwa makini  Mwenyekiti wa kitongoji na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo walipo kuwa wakimuelezea hali halisi ya maendeleo ya elimu ya kijiji cha Kadodo
Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi akimkabidhi kadi ya CHADEMA aliyekuwa mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kododo jimbo la Mvomero, bwana Charles Kiwaga. Wengine ni wanachama wapya wa CHADEMA tawi la Kododo Mvomero.
 
Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM kata ya Muhonda akieleza jinsi alivyokunwa na sera za CHADEMA zilizoelezwa na katibu Mkuu wa BAVICHA katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kichangani.

Wednesday 22 August 2012

Dr. Slaa na Rasilimali za Taifa



Katibu Mkuu wa CHADEMA Dr Wilbrod Slaa amelitaka Jeshi la Polisi kutumia fedha na uwezo wake kulinda Rasilimali za Taifa sio kupambana na CHADEMA

Tuesday 21 August 2012

MAHAKAMA YATENGUA UBUNGE JIMBO LA IGUNGA

Dr Kafumu akiwa na Katibu Mkuu wa CCM Ndg. Mkama
Mahakama yamvua ubunge Dk. Kafumu, uchaguzi haukuwa huru na haki
  • Chadema wafurika mahakamani, vigogo CCM wamtelekeza Dk. Kafumu
  • Dk. Slaa asema ni hukumu ya kihistoria, Rage chupuchupu kwenda jela

Tuesday 14 August 2012

CHADEMA KUWASHA MOTO KATIKA MJI WA READING SIKU YA TAREHE 26/08/2012

UK
Ili kufikia malengo yetu ya kuzunguka kwenye Miji mbalimbali ya UK kuhamasisha Watanzania waishio uk kujiunga na Chadema, kueneza kampeni ya m4c na  kufungua matawi mengine, Tawi la Chadema London linapenda kuwatangazia Watanzania wote waishio katika Mji wa Reading na maeneo ya jirani kuwa kutakuwa na mkutano mkubwa wa M4C UK utakao fanyika Tarehe 26/08/2012 siku ya Bank holiday.
Dhumuni  la mkutano huo ni kuwahamasisha Watanzania waishio UK kujiunga na chama, kushiriki katika harakati za mabadiliko, kusajili wanachama wapya, kuchagua  wawakilishi wa muda kutoka mji wa Reading pamoja na kuanzisha mfuko wa kufa na kuzikana kwa manufaa ya watanzania wote.
Tumekusudia kuanzisha Mfuko wa kufa na kuzikana kwa sababu mpaka hivi sasa Mtanzania akifariki akiwa  UK hakuna taasisi wala ofisi yoyote inayotoa msaada. Jukumu ambalo kwa muda mrefu Serikali yetu kupitia ubalozi umelipuuzia na kushindwa kulisimamia na kulishughulikia. 

Mfuko huu utasaidia katika kumsafirisha Marahemu na Mfiwa pamoja na kusaidia kushughulikia matatizo na usumbufu utakaojitokeza  baada ya mtu kufariki dunia na kusaidia matatizo mbalimbali yakiwemo majanga ya dharura.
Pia katika mkutano huo wanachama mbalimbali wa CCM walio na uchungu na nchi yetu na wanaopenda maendeleo na  mabadiliko ya kweli watapewa nafasi ya kujiunga na Chama cha Demokrasia na Maendeleo kama sehemu moja wapo ya  kampeni yetu ya Kuvua Gamba na Kuvaa Gwanda ukiwa Ughaibuni.
Mkutano utafanyika siku ya Tarehe 26/08/2012, Kuanzia saa saba mchana mpaka saa kumi na mbii jioni.

Risc Reading International Solidarity Centre,
35-39 London Street,
Reading, RG1 4PS

 Watanzania wote, marafiki na wadau mbali mbali  wa maendeleo na mabadiliko ya kweli mnakaribishwa sana.  
Huu ndio wakati wa mabadiliko,  kusimama na kusema tumechoka!
KWA MAELEZO ZAIDI WASILIANA NA;

MWENYEKITI: Chris Lukosi 07903828119,
KATIBU MWENEZI:  Chris Chagula 07405889880
au
Tutumie email kupitia chademauk@gmail.com

HATULALI MPAKA KIELEWEKE!!!!!!!!!!!

Peooooople's Power




Monday 13 August 2012

MATUKIO MBALI MBALI KATIKA SIKU YA UFUNGUZI WA TAWI LA CHADEMA LONDON

VUA GAMBA VAA GWANDA UGAIBUNI

Katika Ufunguzi wa Tawi la CHADEMA London Wanachama mbalimbali wa Chama Cha Mapinduzi walijitokeza kurudisha kadi za CCM na kujiunga rasmi na CHADEMA. Wanachama hao walikabidhiwa kadi za uanachama na Mhe. Lema Mjumbe wa Kamati Kuu Chadema Taifa katika Kampeni Maalumu ya Vua Gamba Vaa Gwanda ukiwa Ugaibuni, Ili kuwapa nafasi watanzania waishio nje ya nchi kulivua Gamba, kuleta mabadiliko , kushiriki katika siasa, na harakati za kulikomboa Taifa kutoka katika utawala wa kifisadi, onyonyaji, uonevu na ahadi za uongo za CCM.


Mhe. Lema na Mwenyekiti wa Muda wa Chadema Lodon Chriss Lukosi wakionyesha baadhi ya kadi na Tshirt zilizorudisha na wanachama wa CCM
Mmoja aliyekuwa Mwanachama na Mkereketwa wa CCM toka Mwaka 1984 Ndg. Christopher Chegula akirudisha Tshirt na Kadi ya CCM kwa Mhe. Lema
Mhe. Lema akimkabidhi kadi ya Uanachama wa CHADEMA Christopher Chegula

Bi. Jessca Maduhu akipokea kadi ya uanachama wa chadema kwa furaha kutoka kwa Lema

Mwanachama Mpya akikabidhiwa kadi yake

Jessica akipokea kadi yake ya CHADEMA

Mmoja ya wanachama waliokabidhiwa kadi na Mh Lema

Esther baby Cuthbert akionyesha kadi yake mpya ya Chadema



VIONGOZI WA MPITO WALIOCHAGULIWA KULIONGOZA TAWI LA CHADEMA LONDON

Mkutano wa ufunguzi wa Tawi la Chadema London ulikwenda sambamba na uchaguzi wa viongozi wa mpito wa Tawi watakao ratibu na kusimamia shughuli  mbalimbali za chama kwa muda, uchaguzi uliongozwa na kusimamiwa na Mh Godbess Lema ambaye ni mjumbe wa Baraza Kuu la Chadema Taifa.
Viongozi waliochanguliwa kuratibu na  kuongoza shughuli za  chama kwa muda ni wafuatao;

Chris Lukosi - Mwenyekiti

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU