Thursday 23 August 2012

Mwalimu mmoja wanafunzi 652

Akiwa katika Oparation Sangara inayoendelea hivi sasa nchini, Mwenyekiti wa Baraza la vijana la Chadema, Bwana Deogratias Munishi amegundua shule ambayo inawanafunzi 652 na Mwalimu mmoja tu. Shule hiyo ipo katika Kijiji cha Kadodo Kata ya  Luale, Mvomelo  Mkoani Morogoro.  Hii ndo hali halisi ya elimu Tanzania baada ya miaka 50 ya uhuru, chini ya utawala wa CCM. 
 
Mwenye shati la rangi ya udongo na suruali nyeusi ndiye Mwalimu Mkuu na Mwalimu pekee wa Shule ya Msingi Kododo iliyopo kata ya Luale, Mvomelo Mkoani Morogoro. Shule hiyo inawanafuzi 652.
 
 
Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi akiwasikiliza kwa makini  Mwenyekiti wa kitongoji na Mwalimu Mkuu wa shule hiyo walipo kuwa wakimuelezea hali halisi ya maendeleo ya elimu ya kijiji cha Kadodo
Katibu Mkuu wa BAVICHA Deogratias Munishi akimkabidhi kadi ya CHADEMA aliyekuwa mwenyekiti wa serikali ya kitongoji cha Kododo jimbo la Mvomero, bwana Charles Kiwaga. Wengine ni wanachama wapya wa CHADEMA tawi la Kododo Mvomero.
 
Aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM kata ya Muhonda akieleza jinsi alivyokunwa na sera za CHADEMA zilizoelezwa na katibu Mkuu wa BAVICHA katika mkutano wa hadhara katika kijiji cha Kichangani.

1 comment:

  1. M4C kwa kwenda mbele na Rais WA wanyonge ana weza jishindia Tuzo Ya AMANI duniani Hii ni kudhihirisha kwamba UKAWA taifa kubwa

    ReplyDelete

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU