Saturday 6 October 2012

Hivi karibuni Waziri wa Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi Prof. Anna Tibaijuka na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dkt. Terezya Huvisa walitoa tamko kwamba nyumba zote zilizojengwa kando kando ya fukwe za bahari na mito zitabomolewa, bila wamiliki kulipwa fidia kutokana na kukiuka Sheria za Ardhi na Mazingira za mwaka 1992, 1995 na 2004.
Kauli hiyo ilitokana na ukweli kwamba imekuwa ni jambo la kawaida kwa watu wenye nguvu ya fedha kuharibu mazingira kwa makusudi pasipo kujali athari ambazo zinaweza kutokea sasa na baadae kwa wakazi wa maeneo husika, jamii inayowazunguka na taifa kwa ujumla!
Kwa watu wengi, kauli ya mawaziri hao ilionekana kama ni hatua muhimu sana katika kulinda mazingira ya fukwe zetu na jamii nzima hasa kutokana na umuhimu wa kulinda mazingira katika wakati huu wa athari za mabadiliko ya tabia nchi.
Lakini baadhi yetu tuliona kama ni mwendelezo wa kauli za Serikali ambazo utekelezaji wake ama huwa ni wa mashaka au ukitekelezwa basi utekelezaji wake hutawaliwa na upendeleo wa hali ya juu kwa watu wenye fedha na nafasi kubwa serikalini (vigogo).
 
Moja kati ya nyumba iliyotakiwa kubomolewa imejengwa kwenye viwanja namba 2019-2020 Kawe Beach, katika fukwe za Bahari ya Hindi. Viwanja ambavyo vilipatikana kwa ushirikiano wa Mchungaji Lwakatare na tapeli maarufu wa Ardhi jijini Dar es salaam, anayejulikana kwa jina la Frank Mushi.
Ikumbukwe kwamba katikati ya mwezi Julai, 2012 wananchi waliojenga nyumba katika maeneo yanayosemekana ni tengefu ya Jangwani Beach, Mto Ndumbwi na Mto Mbezi walivunjiwa nyumba katika operesheni iliyoendeshwa na Baraza la Mazingira la Taifa (NEMC).
Operesheni ambayo ilihusisha takriban nyumba 15 na kuta ( fences) 8. Katika nyumba hizo, mojawapo iliyotakiwa kuvunjwa ni ya Mchungaji Getruda Lwakatare.
Lakini kwa sababu ambazo wahusika, akiwemo yeye mwenyewe na serikali, wanazifahamu, nyumba yake haikuguswa! Wakati wananchi wanaofahamu ukweli wa mambo, wakiwa bado wanahoji chinichini juu ya upendeleo wa kitabaka ulio wazi, hivi karibuni wameshuhudia kupitia njia mbalimbali za upashanaji habari, ikiripotiwa kuwa Mchungaji Lwakatare (Mchungaji wa Kanisa la Assemblies of God na Mbunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ) amehamia kwenye nyumba yake mpya. Nyumba ambayo ilipaswa kuwa imebomolewa kwa sababu imejengwa kwenye viwanja ambavyo ni kinyume cha sheria kujenga katika maeneo hayo.
Kuvunja sheria kwa uwazi namna hii, huku wengine wakichukuliwa hatua kwa kuvunja sheria hiyo hiyo, si tu ni ’double standards’, bali kunaweza kutafsiriwa ni kuitia serikali mfukoni. Kitu kibaya zaidi ni kwamba kiongozi huyo alishataarifiwa tangu mapema juu ya ubatili wa kujenga katika eneo hilo, kupitia kwa huyo Frank Mushi kabla hata ujenzi wa nyumba hiyo haujaanza.
 
Ikumbukwe pia kuwa viwanja hivyo vilipatikana na ujenzi huo kuwezekana baada ya eneo la bahari na mto kujazwa kifusi na mawe! Kwa kutambua kuwa kuendelea na ujenzi katika eneo hilo ni kuvunja sheria za nchi zinazohusu utunzaji wa mazingira kwa manufaa ya jamii nzima, Mchungaji Lwakatare aliendelea kwa kujiificha nyuma ya mgongo wa huyo Mushi, akijifanya hahusiki kabisa na kilichokuwa kikiendelea katika eneo husika. Uthibitisho wa ubatili wa kujenga katika viwanja husika: 1) Tarehe 4/1/2011 Wizara ya Ardhi kupitia barua yenye Kum. Namba LD/297571/18 waliandika barua kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni kuhusiana na uvamizi wa kiwanja nana 2019 na 2020 Mbezi Kawe. Barua husika pamoja na mambo mengine ilibainisha kwamba wizara imefanya ukaguzi katika viwanja tajwa, baada ya kupata malalamiko juu ya uharibifu wa mazingira unaoendelea katika eneo hilo. Na kwamba ukaguzi walioufanya umeonesha kuwa ujenzi unaofanyika katika eneo husika hauruhusiwi na unakiuka Tangazo la Serikali (GN) No. 76 ya mwaka 1992.
 
Kupitia barua hiyo, wizara ilimtaka Mkurugenzi wa Halmashauri kuchukua hatua za kubomoa/kuondoa uendelezaji batili uliokuwa ukifanyika katika viwanja Na 2019 na 2020 Mbezi Kawe. Barua hiyo ilisainiwa na Bwana Sadoth K. Kyaruzi, kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara. 2) Uthibitisho mwingine ni barua ya tarehe 30/9/2011 kutoka NEMC kwenda kwa Bwana Frank Mushi. Barua husika, ilitoa maelekezo kwa Mushi kuvirudisha katika hali yake ya kawaida, viwanja namba 2019-2020 kwa mujibu wa vifungu 55(2) (a) (e), (3) na 151 (1) ,(2) (a), (b), (3) ,(4) (b) na (f) vya Sheria ya Mazingira, sura 191 ya mwaka 2004.
Barua husika inabainisha kwamba timu ya wataalam toka Baraza la Mazingira (NEMC), Wizara ya Maji, Wizara ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Halmashauri ya Jiji la Dar es salaam na Manispaa ya Kinondoni ilitembelea eneo husika kufuatia malalamiko kutoka kwa viongozi na wakazi wa Kawe Beach.
Timu hiyo ilibaini kwamba eneo la Mto Ndumbwi, pamoja na bahari lilikuwa linajazwa mawe na vifusi hali iliyosababisha kupatikana kwa viwanja na 2019 na 2020. Ambapo ndani ya viwanja hivyo lilikuwa linajengwa jumba kubwa kinyume kabisa na vifungu 55(2)(a) , 55(2) (b) , 55(2)(d) na 55(2)(e) vya Sheria ya Mazingira. Ilibainika pia kuwa mikoko ilikatwa kinyume na s.63(1) ya Sheria ya Mazingira. Kwa mujibu wa nyaraka nilizonazo, yafuatayo yalijitokeza i) Timu ya wataalam ilibaini kwamba, tayari Wizara ya Maliasili na Utalii ilishatoa zuio la ujenzi katika eneo husika. ii) Manispaa ya Kinondoni, mara kadhaa iliweka zuio la uendelezaji na kutoa amri kwa ’mmiliki’ wa eneo husika kubomoa, lakini mmiliki huyo alipuuza amri hiyo na kuendelea na ujenzi! iii) Ilitolewa amri ya Mahakama, tarehe 5/4/2011 kumtaka Bwana Mushi asiendelee na ujenzi. Amri hiyo ilipuuzwa na ujenzi ukaendelea. Baraza la Mazingira lilimwagiza tena, Bwana Mushi:-2) Kuvunja majengo yote yaliyoko kwenye viwanja vyenye mgogoro. 3) Ndani ya siku saba, tokea amri husika kutolewa (amri ilitolewa 30/9/2011) awe ametoa mawe na vifusi vyote vilivyoharibu mkondo wa maji na bahari na kuurudisha mto na bahari katika hali yake ya kawaida. 4) Ndani ya siku 30 chini ya usimamizi wa Wizara ya Maliasili na Utalii kuhakikisha kwamba mikoko yote iliyokatwa imerudishwa katika hali iliyokuwa awali. Kwa gharama za Bwana Mushi. Licha ya amri zote hizo, mazuio yote hayo, matamko ya mawaziri yaliyotawaliwa na mbwembwe nyingi, ujenzi uliendelea, nyumba imekamilika. Sasa inatumika.
Wakati kigogo huyo amehamia kwenye nyumba yake kwa matangazo na mbwembwe, Mto Ndumbwi, bahari na mazingira kwa ujumla yameharibiwa vibaya! Bila kusahau kuwa wananchi wengine wamebomolewa nyumba zao kwa kutumia sheria hizo hizo. Kwa mujibu wa Sheria ya Mazingira, Sura 191 ya mwaka 2004, Fungu 57(1) hairuhusiwi kufanya shughuli zozote za kudumu za kibinadamu ndani ya mita 60 ambazo kwa asili yake zinaweza kuhatarisha au kuathiri vibaya ulinzi na utunzaji wa mazingira, utunzaji wa bahari, kingo za mto, bwawa au mwambao wa asili wa ziwa. Halikadhalika, Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999 ( Sura 113) Fungu 7 (1) (d) inabainisha kwamba eneo lolote lililo ndani ya mita 60 kutoka kingo ya mto na bahari linatakiwa kutangazwa kama ardhi hatari au kuhifadhiwa.
Na pale inapotokea kuwa masharti ya sheria moja yanapingana na masharti ya Sheria ya Mazingira, kuhusu mambo yanayohusu usimamizi wa mazingira, Sheria ya Mazingira ndiyo hutumika, kwa mujibu wa Fungu 232 la sheria ya mazingira sura Kutokana na hali hii serikali inatakiwa kujinasua katika mwendelezo wa tafsiri wanayoipata wananchi kuwa imetekwa na kuwekwa mfukoni na watu wachache wenye uwezo. Maana wanaona kuwa huu ni mwendelezo wa serikali kuwa na kigugumizi pale sheria zinapovunjwa na vigogo serikalini au watu wenye fedha wanaoshirikiana na baadhi ya viongozi wa serikali na chama tawala kufanya ufisadi. Wameona mambo ya namna hii mara kadhaa, ikiwemo serikali kushindwa kuwachukulia hatua waliohusika na kashfa kubwa za ufisadi kama ’akina’ Kagoda na wenzake (EPA), Richmond na kashfa nyingine nyingi. Kwamba sasa inazidi kuonekana dhahiri kuwa kuna watu wako juu ya sheria za nchi, huku wanyonge wakishughulikiwa.
Ni wakati mwafaka sasa kwa mawaziri wanaohusika na masuala ya ardhi na mazingira kuwaeleza Watanzania kulikoni wananchi wa hali ya chini kuvunjiwa nyumba zao kwa kigezo cha kuvunja sheria wakati huo huo Mchungaji Lwakatare (kigogo) ambaye uharibifu wake ni wa hatari kuliko hata hao waliovunjiwa akitamba mtaani kwamba yeye yuko juu ya sheria na hakuna mamlaka yoyote yenye uwezo wa kumzuia kufanya alichofanya! Ni aibu kwa Taifa kuwa na viongozi wa aina hii! Viongozi ambao wako tayari kutumia fedha, hila, mamlaka na dhamana za uongozi walizopewa, kuhalalisha haramu, ni janga kwa mstakabali wa taifa letu!
 
Waziri Kivuli, Wizara ya Ardhi ,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Imetolewa Dar es Salaam na;
Halima Mdee (MB)

Waziri Kivuli, Wizara ya Ardhi , Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Picha za M4C Terrat Simanjiro

Kamanda Lema akitoa kadi kwa wananchi


Jackson Makala na James Olle Millya




Friday 5 October 2012

DAR NI SISI- BAADHI YA WANANCHI WAKIELEZEA HALI HALISI YA MAISHA YA DAR



VIDEO BY TWAWEZA ORG.

Sumaye ateta na Chadema


NI KUHUSU MUSTAKABALI WAKE KISIASA

SIKU chache baada ya kushindwa katika uchaguzi wa ndani kwenye nafasi ya Ujumbe wa Halmashauri Kuu ya CCM (Nec), Waziri Mkuu Mstaafu, Frederick Sumaye amekutana na viongozi wa Chadema ikidaiwa kuwa ni kujadili pamoja na mengine, uwezekano wa kuhamia huko ili agombee urais katika Uchaguzi Mkuu ujao 2015.

 
Sumaye ambaye anatajwa kuwa alikuwa na mpango wa kuwania urais kupitia CCM, alishindwa katika uchaguzi wa kuwania ujumbe wa Nec, baada ya kupata kura 481 dhidi ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji), Dk Mary Nagu aliyepata kura 648.
 
Taarifa zilizothibitishwa na baadhi ya viongozi wa Chadema, zimeeleza kuwa Sumaye hakuridhishwa na mchakato wa uchaguzi huo wa Nec na kwa matokeo hayo, alikutana na viongozi wa Chadema kujadili mustakabali wake kisiasa.
 
Jana, mjumbe mmoja wa Kamati Kuu ya Chadema, ambaye aliomba jina lake lisiandikwe gazetini, alithibitisha Sumaye kukutana na viongozi wa Chadema. Hata hivyo alisema hawajafikia mwafaka.
 
Alisema mawasiliano ya Chadema na Sumaye yalianza mara tu baada ya matokeo ya uchaguzi huo uliofanyika Septemba 30, mwaka huu yaliyomwengua kigogo huyo kwenye kinyang’anyiro hicho.
 
“Ni kweli kuna watu wa CCM tumewasiliana nao baada ya uchaguzi ule (wa Nec) na Sumaye tunawasiliana naye pia lakini siwezi kusema tumefikia wapi,” alisema mjumbe huyo na kuendelea: “Suala kwamba amekubaliwa kujiunga na Chadema au la, nadhani huu ni uamuzi wake. Ninachoweza kusema ni kwamba vikao vilikuwepo na vinaendelea kukaliwa.”
Alisema baada ya matokeo ya Hanang’ na hali ya kisiasa ndani ya CCM, Chadema kimekuwa kikiwasiliana na Sumaye na kikubwa ambacho kinajionyesha ni kada huyo wa CCM kutoridhishwa na hali ya mambo ndani ya chama chake.
 
Mjumbe huyo wa Chadema alisema chama hicho Wilaya ya Hanang’ kinaandaa mkutano maalumu wa kuwapokea wanachama wapya wa CCM, wengi wao wakiwa baadhi ya walioanguka kwenye uchaguzi wa Nec wilayani humo.

Habari zaidi zimeeleza kuwa Chadema kimepanga siku yoyote juma lijalo, kuwapokea wanachama wapya kutoka CCM, baadhi wakiwa wale walioshindwa kwenye uchaguzi wa ndani ya chama hicho uliofanyika wilayani Hanang’.

Mmoja wa watu wa karibu na Sumaye alisema anachojua ni kwamba Chadema wanamtaka Sumaye na siyo Sumaye kukitaka chama hicho cha upinzani.

“Wamekuwa wakimfuatafuata mara nyingi na mazungumzo ya aina hiyo si mageni baina ya Sumaye na Chadema. Ila ninachoweza kusema, safari hii chochote kinaweza kutokea kutokana na hasira alizonazo (Sumaye). Ngoja tusubiri, atafanya mkutano na waandishi Jumapili.”

Sumaye, Mbowe wazungumza
Alipoulizwa kuhusu madai hayo, Sumaye alisisitiza kuwa atazungumzia masuala yote yanayohusiana na uchaguzi huo wa Hanang’ atakapokutana na waandishi wa habari, Dar es Salaam.

 
“Nitakutana na waandishi wa habari kuzungumzia kilichotokea naomba tu mwendelee kunipa muda,” alisema Sumaye na kuongeza kuwa alikuwa akijiandaa kwa safari ya kwenda Dar es Salaam.
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema asingependa kuzungumzia suala hilo kwa kuwa yeye si msemaji wa Sumaye... “Sitaki kumzungumzia Sumaye. Mimi si msemaji wake. Tumsubiri yeye azungumze kuhusu hilo.”
Kada wa CCM Hanang’ anena

Katika hatua nyingine, aliyekuwa Mwenyekiti wa CCM Hanang’, Goma Gwaltu amekionya chama hicho kuwa kisipodhibiti vitendo vya rushwa katika chaguzi zake, kitakufa.
Gwaltu alisema jana kwamba kwa mazingira yaliyopo sasa ndani ya CCM bila hatua kali kuchukuliwa, kiongozi asiye na fedha hawezi kushika uongozi na ndiyo sababu anaungana na wana-CCM wengine katika wilaya hiyo, ambao wanafikiria kukihama chama hicho.
 
“Kama wewe una nia ya kuendelea na siasa siyo rahisi kushinda hapa Hanang’ ukiwa hukubaliani na watu fulani, sasa mimi naona ni bora tu kutafuta chama kingine kwani siyo dhambi,” alisema Gwaltu bila kuwataja ambao wanataka kuhama CCM.
 
Hata hivyo, Gwaltu alisema kwa upande wake, hafikirii kuendelea na mambo ya siasa wala kulalamika makao makuu ya CCM kuhusiana na alichokiita hujuma alizofanyiwa

Kwa habari kamili tembelea:
 

MBUNGE WA MUSOMA MJINI, VICENT NYERERE (CHADEMA) AMETOA RUNIGA KWA WAFANYABIASHARA WA SOKO KUU LA MUSOMA ILI WAWEZE KUPATA HABARI WAWAPO KAZINI

MBUNGE wa Musoma Mjini, Vicent Nyerere (CHADEMA), amekabidhi runinga 10 kwa wafanyabiashara wa soko kuu la Musoma mkoani Mara. Mbunge huyo alikabidhi runinga hizo jana, zenye thamani ya Sh milioni 9, katika eneo la ndani ya soko hilo lenye wafanyabiashara wengi.

Nyerere alisema kuwa, wafanyabiashara wa sokoni wamekuwa wakikosa haki ya kupata habari za uhakika, kutokana na kushinda kutwa nzima sokoni.

“Wafanyabiashara wa sokoni ni watu wa kuhangaika, hawana televisheni katika maeneo yao ya kazi na wanaporudi nyumbani, hupata habari za kusikia kwa watu,” alisema.

Amesema runinga hizo zitawasaidia kupata habari za mambo mbalimbali yanayoendelea nchini, ikiwa ni pamoja na uendeshwaji wa vikao vya Bunge.

“Wanapitwa na mambo mengi, vikao vya Bunge huanza asubuhi muda ambao wafanyabiashara hawa wapo sokoni, wanakosa haki ya kupata habari,” alisema.

Akipokea runinga hizo kwa niaba ya wafanyabiashara, Ofisa Biashara wa Manispaa ya Musoma, God Machumu, alimpongeza mbunge huyo kwa kutimiza ahadi yake kwa wananchi.

Mbali ya kupokea runinga hizo, wafanyabiashara hao walimweleza mbunge huyo changamoto mbalimbali wanazokabiliana nazo katika soko hilo.

Miongoni mwa changamoto hizo, ni pamoja na usumbufu nyakati za masika, kutokana na soko hilo kujaa maji, hali inayosababishwa na soko hilo kukosa mitaro ya maji.

Tatizo la ulinzi katika soko hilo limeelezwa kuwa, kikwazo katika maendeleo ya wafanyabiashara hao kwa madai kuwa, wamekuwa wakiibiwa mali zao kutokana na kutokuwepo kwa ulinzi wa kuaminika.

Thursday 4 October 2012

Dr Slaa kutikisa Arusha Siku ya Jumamosi

 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) anatarajiwa kuhutubia mkutano mkubwa wa hadhara katika jiji la Arusha siku ya Jumamosi tarehe 06.10.2012 kuanzia saa 8 mchana. Pamoja na mambo mengine Kiongozi huyo wa CDM pia atatumia mkutano huo kuzindua rasmi kampeni za udiwani katika kata ya daraja mbili,uzinduzi huo utafanyika katika viwanja vilivyopo mtaa wa NDARVOI.

Tayari kuna hekaheka kubwa katika jiji la Arusha kuhusiana na mkutano huo ambapo mazungumzo ya watu mbalimbali yanazungumzia mkutano huo unaotarajiwa kuwa gumzo.

Taarifa za awali zinasema mkutano huo pia utatumika kufuta nyayo za chama cha CUF ambacho kilisomba watu Dar-es-Salaam kwenda kuwahutubia Arusha ili kuepuka aibu ya kukosa watu.Pia inadaiwa wananchi wa Arusha wamedhamiria kuonyesha dunia uungaji mkono wao kwa chama cha CDM.

Zitto Kabwe Achangia Bima Ya Afya Ya Mjane Wa Mwangosi Na Wanae Kupitia NSSF

KATIKA siku ya mwisho ya harambee ya kumchangia mjane wa marehemu Daud Mwangosi, Ndugu Zitto Kabwe amejitolea kumchangia mjane wa marehemu kwa kumlipia ada ya uanachama wa Mfuko wa Hifadhi ya Kijamii (NSSF) kwa kila mwezi na kwa miaka mitatu mfululizo.

" Nimeona nami niunge mkono harambee hii. Pamoja na michango ya fedha iliyotolewa kumsaidia mjane kuanzisha mradi wa kujikimu, mimi naona ni muhimu pia mjane akawa na hakika ya huduma ya afya yake na watoto wake wanne. Hivyo, mchango wangu utakuwa ni kwenye eneo hilo la Bima ya Afya na kwa miaka mitatu." Anasema Zitto Kabwe alipoongea na Mjengwablog.com, mtandao wa Kijamii ulioratibu harambee ya mjane wa Daud Mwangosi.

Hii ni mara ya pili kwa Ndugu Zitto Kabwe kuchangia kwenye masuala ya kijamii kupitia mtandao wa kijamii wa Mjengwablog.com, mara ya kwanza ni alitoa mchango wake pale Mtandao wa Mjengwablog.com ulipoendesha harambee ya kuwachangia watoto wa Somalia waliokuwa katika hatari ya kufa kwa njaa. Katika harambee iliyomalizika Jumapili ya Septemba 30 mwaka huu na iliyochukua kipindi cha mwezi mmoja,zaidi ya shilingi milioni tano na nusu zimekusanywa.

Mchango huo wa Ndugu Zitto Kabwe una maana mjane wa marehemu ataweza kuwa na hakika ya yeye na watoto wake wanne kupata huduma za afya bila kufikiria malipo kwa kipindi cha miaka mitatu. Baada ya hapo,michango ya mjane huyo ya kila mwezi kwa mfuko huo wa hifadhi ya kijamii ( NSSF) ambayo atakuwa akilipiwa na Ndugu Zitto Kabwe itakuwa ni malimbikizo ya akiba yake ambayo mjane atakuwa na uwezo wa kuichukua kama akipenda. Kwa sasa mjane wa Daud Mwangosi hayuko kwenye utaratibu wowote wa Bima ya Afya, kwake yeye na wanawe.

Harambee ya mjane wa Daud Mwangosi iliyoendeshwa kwa uwazi kwa njia ya MPESA, TigoPesa, Airtel Money, NMB Mobile na Western Union ilimwezesha mchangiaji kuliona jina lake na mchango wake kwenye orodha ya wachangiaji iliyokuwa ikiwekwa mtandaoni kila siku.

Michango ilikuwa ni hiyari, hakuna aliyeombwa kutoa na utaratibu haukuruhusu ahadi za kuchangia, bali, mwenye nacho alitoa na hapo hapo kuorodheshwa kama mchangiaji. Utaratibu haukuruhusu pia michango iliyofungamana na siasa za vyama.

Hatua hiyo ya uwazi na kutanguliza ubinadamu na si itikadi kwenye uchangiaji imechangia kupelekea Watanzania wengi wa kada zote, kwa namna moja au nyingine kushiriki kwenye kuchangia. Kuna waliochangia shilingi elfu moja na kuna waliochangia mpaka shilingi milioni moja.

Ari hii ya Watanzania kujitolea kusaidiana kwenye hali kama iliyomkuta mjane wa Daud Mwangosi imedhihirisha umoja na upendo tulionao kama Watanzania, na pia imeonyesha jinsi tunavyoijali amani yetu na hivyo jamii, kupitia michango hii, imeonyesha pia kwa vitendo, dhamira ya kulaani kwao vitendo vya maovu na vinavyotokana na matumizi ya nguvu yasiyo ya lazima kama kile kilichomtokea mwandishi Daud Mwangosi.

Baadhi ya watu maarufu katika jamii waliojitokeza kwa hiyari yao kumchangia mjane wa Daud Mwangosi kupitia mtandao wa kijamii wa Mjengwablog.com ni pamoja na Shy- Rose Bhanji, Ananilea Nkya, John Bukuku ( Mmiliki wa Fullshangwe.blog) na Ndugu Mobhare Matinyi aliyepata kuwa mhariri wa gazeti la Majira.

Michango kwa mjane wa Daud Mwangosi itaingizwa kwenye akaunti ya mjane ya CRDB, Iringa leo alhamisi, Oktoba 4, 2012. Vielelezo vya kibenki vitawekwa kwenye mtandao wa Mjengwablog.com kwa kila mmoja kuona jumla iliyowasilishwa kwa mjane na orodha ya majina ya wachangiaji.

Chanzo: http://www.mjengwablog.com/2012/10/zitto-kabwe-achangia-afya-ya-mjane-wa.html
MIAKA michache iliyopita niliandika makala ndefu sana nikiwashauri Watanzania wenzangu waliokuwa wanapigania sana vyama viungane ili kuwa na upinzani dhidi ya chama tawala na hatimaye kukiangusha chama tawala.
Naomba nikupitishe kwa kifupi sana msomaji wa kona hii kwenye makala ile ya Oktoba 8, 2008.

Niliamua kutumia makala nzima kueleza kwa kinagaubaga mawazo yangu kuhusu ushirikiano wa vyama vya upinzani ambao ulikuwa ukipigiwa upatu sana na Watanzania kwa muda mrefu. Siku hiyo niliwaambia kwamba ni vema ushirikiano wa vyama vinne vya upinzani (CHADEMA, CUF, NCCR-MAGEUZI na TLP) ukavunjika kwa masilahi ya taifa.


Nilieleza jinsi vyama vya upinzani vilivyoungana Kenya lakini baada ya kuing’oa KANU kulizuka mgogoro wa chama hiki kudai kupewa mawaziri wachache, kile kikidai kunyimwa wizara nyeti, hiki hapa kikidai makubaliano yamekiukwa na mambo kadha wa kadha mpaka wakagombana. Walisambaratika na kumlazimisha Rais aliyetokana na upinzani kuanzisha ushirikiano mpya na Rais aliyeondoka madarakani na hivyo kufifisha vita dhidi ya ufisadi na kusababisha serikali iliyokuwa madarakani ionekane ya ufisadi sawa na ile serikali iliyokuwa imepita.


Huo ndiyo ushirikiano wa vyama vya upinzani unaotafutwa na Watanzania?


Niliwatahadharisha Watanzania kwamba hatuhitaji ushirikiano wa vyama vya upinzani wenye lengo la kuing’oa CCM madarakani. Tunahitaji Tanzania mpya yenye kutoa fursa kwa kila raia kufaidi rasilimali za nchi hii na kujiletea maendeleo bila kujali katokea kundi gani.


Ushirikiano wa CHADEMA, CUF, NCCR na TLP hautafanikisha hayo.


Niliwashauri Watanzania tuwaruhusu wapinzani wavunje ushirikiano wao halafu wajijenge kama chama kimoja kimoja na ndipo tutakapoona chama chenye mwelekeo wa kuleta maendeleo tukipe kura.


Siku hiyo nilisema: “Natamani chama kama CHADEMA, ambacho kimejipambanua hivi karibuni kuwa chama makini chenye sera nzuri zilizopata kusifiwa hata na Mwalimu Nyerere wakati wa uhai wake na ambacho hivi karibuni kimewaonyesha Watanzania kwamba kumbe inawezekana kuiondoa CCM na tukaongozwa na chama kingine na kujipatia maendeleo ambayo hatukuwahi kuyaota wakati wote wa CCM, kipate kukubalika toka kwa Watanzania.


Wakipokee na kukipa nafasi ya kujipanua na mwaka 2010 kuwe na uchaguzi wenye ushindani kama tuliokuwa tunaushuhudia Tarime.


Vyama vingine viendelee kusimamisha wagombea urais, ubunge na udiwani kwa kuwa ni haki yao lakini mchuano uwe kati ya vyama viwili kama tulivyoona kule Tarime na hapo ndipo tutakuwa tunaelekea huko kwenye maendeleo.


Hayo yalikuwa baadhi tu ya maneno niliyoyasema wakati huo. Ni kama CHADEMA waliisoma makala ile kwa makini na kuielewa kwa kuwa muda mfupi baadaye walitangaza kuvunja ndoa ya upinzani na kuanza kujiimarisha kama chama peke yake chenye malengo ya kuchukua dola kwa kutumia sera zake chenyewe na kuepuka mtego wa kuungana na baadaye kuanza kupigana ni sera za chama gani kwenye ushirikiano zitekelezwe.


Wakaanzisha kile kilichojulikana kama Operesheni Sangara ambayo kwa kiwango kikubwa ilikidhoofisha sana chama tawala sanjali na vyama vingine vya upinzani.


Watanzania wakaanza kuielewa CHADEMA kama chama. Februari 11, 2009 nikaandika makala nyingine yenye kichwa cha habari, “CHADEMA na CUF wanahitaji msaada wako.”


Katika makala ile nikaomba kura ya maoni ikiwa vyama hivyo viwili viungane ama viendelee kujijenga kila kimoja kivyake! Wengi wakasema kila chama kijijenge kivyake, sababu zilikuwa nyingi na zote niliziandika katika makala iliyofuata.


Operesheni Sangara ilikuwa kama mashambulizi ya anga vitani. Mashambulizi ambayo siyo siri kwamba yamevidhoofisha mno vyama vikubwa kama CCM na CUF.


Ushahidi wa hili ni matokeo ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2010 ambapo CHADEMA ilipaa kutoka majimbo mtano ya ubunge iliyoyapata 2005 mpaka 23 mwaka 2010.


Wabunge viti maalumu kutoka 6 mpaka 25. Halmashauri za wilaya zinazoongozwa na CHADEMA kutoka vitatu mpaka saba.

Kura za urais kutoka laki sita mpaka mpaka milioni 2 na ushee, madiwani idadi ikaongezeka zaidi ya mara tano.
Kuimarika huku kwa CHADEMA hakuwezi kutokea bila kuviathiri baadhi ya vyama.


CCM kwa mfano majimbo yote ya CHADEMA yaliyoongezeka yalitoka mikononi mwa CCM, halmashauri zote zilizoongezeka kuongozwa na CHADEMA zilitoka mikononi mwa CCM, kura za urais zilipoongezeka zilipungua za CCM na CUF, kambi rasmi ya upinzani bungeni sasa ikapokwa mikononi mwa CUF ambayo imeiongoza kambi hiyo tokea mwaka 1995 na uongozi wa kambi sasa ukachukuliwa na CHADEMA.


Ruzuku ya CCM sanjali na ya CUF zinapungua wakati ya CHADEMA ikiongezeka kutoka milioni 60 kwa mwezi hadi milioni 230 kwa mwezi. Watanzania wakazidi kuipenda CHADEMA na wito wangu katika makala ile wa kuwataka Watanzania wakikumbatie hiki chama kama chao na kukiimarisha tayari kwa kukifanya chama mbadala wa kilichoko madarakani ukaonyesha kupokelewa na kutekelezwa barabara.

Safari ya CHADEMA kuelekea Ikulu ikaanza rasmi.


Ulipotokea uchaguzi mdogo Arumeru Magharibi, CHADEMA iliingia kwenye uchaguzi huo na kumbukumbu ya kipigo (hata kama kilikuwa cha haramu kama ilivyothibitishwa na mahakama hivi karibuni). Nikiwa mmoja wa viongozi wa chama tena nikiwa ndiye mwenyekiti wa mkoa wa Arusha ambamo ndimo kulikuwa na uchaguzi huo mdogo wa Arumeru, ilibidi kukaa na kufanya maamuzi.


Jambo la kwanza tulinuia hakuna kushindwa Arumeru kwa kuwa mtanange ilikuwa umekuja nyumbani ingelikuwa ni aibu kushindwa tena hata kama ushindi wa CCM ungelikuwa wa magumashi kama ambavyo imefanya siku zote.


Tukamuacha katibu mkuu wa chama akiwa na makamanda wengine katika kuhakikisha kampeni zinaanza na mikakati mingine ya kawaida ya kampeni zetu inaendelea.


Uongozi wa mkoa ukaungana na Mwenyekiti Taifa, Mkurugenzi wa Raslimali Taifa na Mkurugenzi wa Fedha Taifa, tukakaa pamoja kuandaa mkakati wa pekee wa ushindi ikiwa ni pamoja na kupata fedha na raslimali zingine kwa ajili kuendesha kampeni.


Ni katika kukaa wakati huo ndipo tulipokuja na wazo la M4C ama “Movement for Change” ama “Vuguvugu la Mabadiliko” kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili. M4C ikanuia kukikabidhi chama kwa wananchi. Wazo lilelile nililolizungumza kwenye makala yangu mwaka 2008.


Wanachama wakaipokea M4C nchi nzima. Wakachanga pesa na rasilimali nyingine na kiukweli kilichonishangaza zaidi ni kitendo cha wana CCM wengi wa chini kuipokea M4C na kuipa sapoti kubwa.


Katika uchaguzi wa Arumeru Mashariki wana CCM walifanya kazi ya ziada kuibeba CHADEMA. Walitupatia kura zao na za ndugu zao lakini zaidi walifichua hujuma nyingi sana zilizokuwa zinaandaliwa na CCM juu yetu. Tukapata ushindi wa kishindo!

Tukaikabidhi M4C kwa chama taifa na likawa sasa ni vuguvugu la nchi nzima. Kamati Kuu ikaamua kwa makusudi kuiboresha M4C ili itembee kwa mpangilio nchi nzima. Wakaamua kwamba sasa M4C ya kitaifa izinduliwe Dar es Salaam ili kufuta propaganda ya kwamba CHADEMA ni chama cha kaskazini tu.
Kutoka kwenye uzinduzi Dar es Salaam kwa makusudi kamati kuu ilikuwa imeelekeza M4C ielekee Mtwara na Lindi, eneo la ukanda wa Pwani ya kusini ambako CCM imekuwa ikidanganya watu kwamba CHADEMA haiwezi kwenda kwa sababu ni eneo la Waislam wengi na CHADEMA ni chama cha Wakristo.


Kazi iliyofanywa huko na M4C ya CHADEMA wanaoweza kusimulia vizuri ni kina Bernard Membe, George Mkuchika, Mathias Chikawe, Hawa Ghasia na wenzao ambao walikimbia majimboni kwenda kushuhudia. Kule CHADEMA ilifuta utawala wa CUF na CCM uliodumu miaka mingi.


Ili usipate shida ya kuniamini mimi au wale wasioitakiwa mema CHADEMA, ni vizuri ukaenda mwenyewe kufuatilia na kujua CHADEMA inaendeleaje huko kwa sasa.


M4C inafanyaje kazi. Imegawanywa katika vikosi vinne na awamu nne tofauti.


Kwanza hutangulia kikosi cha tathmini kinachokwenda kukagua hali ya chama na uongozi wa wake.


Hiki huweza kuja na majibu yanayoonyesha chama kiko katika hali gani na ni maeneo gani yanahitaji kuongezewa uzito.


Baada ya ripoti yao huja kikosi cha hamasa ambacho hufanya mashambulizi ya anga kwa njia ya mikutano ya hadhara kwa ajili ya kuhamasisha na kuingiza wanachama wapya.


Baadaye huja kikosi cha tatu ambacho kazi yake ni kusimamia uchaguzi tangu ngazi ya matawi mpaka kata.


Na mwisho huja kikosi cha mwisho ambacho hutoa mafunzo kwa viongozi waliochaguliwa kuwafanya wakijue chama waijue katiba ya chama, kanuni za uendeshaji chama, taratibu na maadili ya viongozi na wanachama ili waweze kuongoza vizuri chama kwa mujibu wa katiba, kanuni na maadili chama. Na vikosi hivyo vinapoondoka, vinaacha viongozi wa matawi na kata wakishuka kuweka kusimika viongozi wa misingi na mabalozi wa nyumba kumi wa CHADEMA. Wapi CCM itaponea? Wapi CUF itatokea? Hapo ndipo CCM ilipokiona kifo chake na CUF ikaanza kunusa kuzidi kudumaa kwake.


Unapomsikia leo Mwenyekiti wa CCM taifa anajiwahi wahi kusema CCM haifi kabla hajaulizwa, ni kile kile alichokisema Ansbert Ngurumo Jumapili iliyopita kwamba ni kama mlevi ambaye amelewa chakali na anatembea barabarani kwa kuyumba yumba na kuanguka hovyo, anapopishana na watu anaona wakimshangaa anaanza kupaza sauti: “Nani kasema mimi nimelewa? Sijalewa mimi!”


Kikwete kasoma nyuso za Watanzania na alipofika ukumbini akasoma nyuso za wajumbe wa Halmashauri Kuu ya chama chake, kama mlevi akaona wajumbe wakishangaa jinsi alivyochoka na chama kinamfia mikononi mwake. Kama yule mlevi akaanza kupaza sauti: “Kina nani wanasema CCM inakufa? CCM haifi bali wanaoiombea kifo watakufa wao na kuiacha imara!”


Naam, kupitia M4C CCM inakiona kifo chake kinavyokuja kwa hakika tena chafanya haraka. CUF nao wanaziona dalili za kunyauka kwani watabaki na mzizi mmoja tu ule wa Pemba ambao kwa kibaiolojia hauwezi kupitisha maji na madini ya chumvichumvi ya kuulisha mti mkubwa wa nchi nzima uitwao Chama cha Wananchi (CUF).


Ndiyo maana M4C ilipohamia Morogoro, Iringa, Dodoma, Singida na Manyara, ilibidi CCM na serikali yake watumie nguvu za dola kuizima na kuifanya isiendelee ili wenyewe wabaki madarakani.


Lakini niliwahi kusema huko nyuma baadhi ya watu wakanishambulia. Kwamba CHADEMA kina mkono wa Mungu maana hata yeye amechoka kuona watanzania wakiteseka hivi, ameleta mkombozi. Mbinu ya kutumia dola imeshindwa baada ya kifo cha Mwangosi. Sasa wamebuni kitu kipya. CCM wanaungana na CUF kuikabili M4C ya CHADEMA.


Ni bahati mbaya kwamba katika mkakati wao wameamua kuanzia Arusha. Walidhani kwa kuwa Arusha ni ngome ya CHADEMA na vijana wa Arusha hawana mchezo linapokuja suala la kutetea chama chao, wakadhani watawachokoza halafu CHADEMA watajibu kwa kuwafanyia vurugu na kisha serikali ya CCM iseme, “Mikutano ya kisiasa kwa sasa imekuwa chanzo cha uvunjivu wa amani.


“Kwa hiyo serikali imesitisha mikutano ya vyama vyote mpaka hapo hali itakapotulia.”


Itatulia lini, anajua waziri wa mambo ya ndani na jeshi lake la polisi na usalama wa taifa. Kwa kufanya hivyo watakuwa wamezuia M4C isiendelee. Ndugu yangu Mtatiro, wewe ni rafiki yangu sana. Nimeandika makala kadhaa kukutetea ulipokuwa unashughulikiwa pale Mlimani kwa sababu za kisiasa. Lakini katika hili sitakubaliana nawe niko tayari uniseme utakavyosema.


Ili kuonyesha kwamba ni mkakati, Mtatiro ulikuwa Dar es Salaam wakati ‘advance team’ yenu ilipokuja Arusha kuhamasisha ujio wa Ibrahim Lipumba, mheshimiwa mwenyekiti wenu taifa. Walifanya mikutano michache, mimi nilishuhudia mmoja tu pale Mbauda Sokoni ambapo walihutubia mkutano uliohudhuriwa na wananchi 11. Walikuwa wakihutubia kwa amani tele. Shida ilikuja pale walipokuta wamachinga wakiwa katika harakati za kujitwalia kwa nguvu kiwanja cha wazi kilichouzwa kifisadi kwa mtu binafsi.


Uuzaji ambao ulisababisha meya wa Arusha wakati huo ajiuzulu. Walikuwa wameziba barabara iendayo Kilombero sokoni. Gari la matangazo la CUF likaja.


Wakawaomba wageuze na kutumia barabara nyingine. Hawakutaka wakawa wanalazimisha kupita pale wakiimba nyimbo za CUF na kuwaonyesha ishara za chama chao.


Wamachinga wachache wakaamua kuwaonyesha alama ya CHADEMA pengine kuwaonyesha kwamba sisi wengine ni wanachama wa CHADEMA kwa hiyo hatuna haja ya kuonyeshwa alama za CUF.


Mtu mmoja aliyekuwa kwenye gari la matangazo la CUF akaamua kuwaonyesha wamachinga wale alama ya vidole vya kuonyesha matusi. Hapo ndipo wamachinga walipokasirika na kuwarushia mawe. Kumbe ni mtego uliopangwa, saa hiyo hiyo Mtatiro akarusha kwenye mitandao kwamba Wanachadema wamewashambulia wana CUF.


Baadaye wameleta Coaster zaidi ya nane kuja kuhudhuria mkutano wao wa Lipumba. Wakiwa njiani huko walipoulizwa na watu ambao hawakujua kama ni CHADEMA wakawa wanasema wanakwenda Arusha kulipiza kisasi cha watu wao kupigwa na CHADEMA. Wamekuja, Lipumba kahutubia hao watu wake aliowatoa Dar es Salaam na wana Arusha wasiozidi 100.


Kahutubia kwa amani kaondoka na hakuna badiliko lolote! Magazeti ya kesho yake hayakupata hata kuiweka habari yao ukurasa wa mbele isipokuwa yale ya wabia wao CCM ambayo yalidiriki kusema eti diwani wa CHADEMA ahamia CUF wakati wakijua huyo mtu alifukuzwa uanachama na CHADEMA na kupoteza hata udiwani. Anakuwaje diwani wa CHADEMA? Kwa hiyo V4C ilijifia kabla hata haijaanza kama walivyotabiri waandishi wenzangu.


Na mkakati wa pamoja kati ya CCM na CUF nao umefeli kabla ya majaribio jijini Arusha. Labda niwashauri wakaanzie huo mkakati Pemba
 

Zitto apeleka hoja bungeni kutaka uchunguzi walioficha mabilioni nje

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe ameiandikia barua Ofisi ya Bunge kuitaarifu nia yake ya kuwasilisha hoja binafsi katika Mkutano wa 11 wa Bunge kuliomba liazimie Serikali iwasiliane na taasisi za kimataifa, hasa benki kusaidia kurejeshwa nchini fedha zote haramu ambazo zimefichwa na Watanzania katika benki za nchini Switzerland na kwingineko duniani.
Taarifa zilizopatikana jana kutoka Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni zimeeleza kuwa Zitto anaomba Serikali ifanye hivyo kwa Benki ya Dunia kupitia taasisi yake ya Stolen Asset Recovery Initiative, kutekeleza jukumu hilo.
Taarifa hizo zimeeleza kuwa katika barua hiyo Zitto anatumia kifungu cha kanuni za bunge namba 55 (1) na (2), na hoja yake itaainisha fedha ambazo Benki ya Taifa ya Switzerland ilitangaza kwamba Watanzania wamezihifadhi, ambazo ni Sh297 bilioni.
Barua hiyo imeainisha kuwa fedha hizo ni sawa na Dola za Marekani 186 milioni na Zitto amebainisha kuwa hoja yake hiyo itaainisha namna na njia ambazo zilitumika kutorosha fedha hizo kwenda katika benki hiyo na nyingine za nje.
Katibu wa Bunge, Dk Thomas Kashillilah alikataa kuthibitisha kupokea barua hiyo badala yake alieleza kuwa hilo ni suala la kiofisi.
"Ni suala la ndani la ofisi, siwezi kueleza kama ni kweli nimepokea au la, isipokuwa suala hilo linafahamika na ofisi ya Bunge ililipokea alipoliwasilisha bungeni hivyo linafanyiwa kazi," alisema Kashillilah.
Mapema mwaka huu, baadhi ya vyombo vya habari likiwamo gazeti hili, vilifichua kuwapo kwa fedha zilizofichwa nchini Uswisi na baadaye ilibainika kwamba fedha hizo ni mali ya Watanzania 27 wakiwamo wanasiasa na wafanyabiashara.
Gazeti hili pia lilibaini kwamba mmoja wa walioficha fedha hizo anamiliki Dola za Marekani milioni 56 (sawa na Sh89.6 bilioni).
Katika uchunguzi wake, Mwananchi limebaini pia kuwa kiasi cha fedha kilichothibitishwa kumilikiwa na Watanzania hao ni jumla ya Dola za Marekani 186 milioni (takriban Sh300 bilioni) kwa viwango vya sasa vya kubadilishia fedha ambavyo ni Sh1600 kwa Dola ya Marekani.
Taarifa hizo zinaeleza kuwa mbali na kigogo anayemiliki Sh90 bilioni, wapo wengine wanne, ambapo anayefuatia anamiliki Dola 30 milioni (Sh48 bilioni), mwingine Dola 20 milioni (Sh32 bilioni) na wengine wawili kila mmoja anamiliki Dola 10 milioni (Sh16 bilioni).
Kwa kuangalia fedha hizo ni dhahiri kwamba vigogo watano tu kati ya kundi la Watanzania 27, wanamiliki Dola 126 milioni (Sh201.6 bilioni) sawa na asilimia 67.74 ya fedha hizo, wakati wengine 22 waliobaki wanamiliki Dola 60 milioni (Sh96 bilioni) sawa na asilimia 32.25.
Habari hizo zilikuwa zikinukuu taarifa ya Benki Kuu ya Uswisi iliyoitoa na kuonyesha kuwapo kwa kiasi cha Sh315.5 bilioni zilizotoroshwa Tanzania na kufichwa nchini humo na vigogo ambao ni wanasiasa pamoja na wafanyabiashara.
Mwananchi

Wednesday 3 October 2012

Vigogo CCM ‘wahamia’ Marekani

• Ni JK, Mkapa, Kinana, Membe na Nape
 
VIGOGO watano wa Chama cha Mapinduzi (CCM), wako nchini Marekani, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Uwepo wa vigogo hao Marekani kwa wakati mmoja, umeibua gumzo nchini hususan kwa mitandao ya makada wa chama hicho wanaotajwa kutaka kuwania urais mwaka 2015.
Vigogo hao ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa, na mjumbe wa Kamati Kuu (CC) na Halmashauri Kuu (NEC), Abdulhaman Kinana, ambaye amepata kuwa kampeni meneja wa marais hao wawili.
Mwingine ni Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernad Membe, ambaye amekuwa akitajwa kuwa mmoja wa makada watakaowania urais mwaka 2015.
Wakati vigogo hao wako nchini Marekani, kigogo mwingine wa CCM, Nape Nnauye, ambaye ni Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, anatarajia kwenda nchini Marekani kesho.
Ingawa vigogo hao wako Marekani kwa shughuli na sababu tofauti, mahasimu wa Waziri Membe kisiasa wamehusisha ziara hiyo ya wazito hao na harakati za urais 2015.
Rais Kikwete yuko nchini Marekani kwa ziara ya kikazi. Rais na ujumbe wake uliondoka nchini juzi na atakuwa hapo kwa siku mbili kabla ya kuelekea nchini Canada kwa ziara nyingine rasmi ya kiserikali.
Habari zinasema kuwa Mkapa na Kinana waliondoka nchini wakati vikao vya mchujo vya CCM vikiendelea mjini Dodoma na wako nchini humo kwa ajili ya shughuli za taasisi ya Mkapa Foundation na Nape anatarajia kwenda kwa shughuli zake binafsi.
Hadi sasa hakuna kada yeyote wa CCM aliyetangaza kuwania urais, lakini mbali ya Membe, duru za kisiasa zinawataja makada wengine wanaotaka urais kuwa ni pamoja na mawaziri wakuu wastaafu, Frederick Sumaye na Edward Lowassa.
Hata hivyo, kasi ya Sumaye kuwania nafasi hiyo imepunguzwa na matokeo ya uchaguzi wa NEC, wilayani Hanang’ ambapo aliangushwa na Dk. Mary Nagu.
Wengine ni Samuel Sitta, Dk. Abdallah Kigoda, Dk. Emmanuel Nchimbi, Dk. Asha Rose Migiro na wengine.
KWA HABARI KAMILI TEMBELEA:
 

Kingunge nusura amng’oe Kikwete

MWENYEKITI wa Chama cha Mapunduzi, Rais Jakaya Kikwete, na sekretarieti yake wameponea tundu la sindano kung’oka baada ya mkongwe wa siasa nchini, Kingunge Ngombale Mwiru, kutangaza mgogoro wa katiba ya chama hicho ambao ungehatarisha nafasi yake.
Kingunge ambaye ameshika nafasi mbalimbali za uongozi nje na ndani ya chama, aliwasilisha hoja hiyo ya mgogoro wa katiba wiki iliyopita wakati wa kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), iliyokuwa na ajenda ya kufanya uteuzi wa majina ya wagombea wa nafasi mbalimbali za uongozi ndani ya CCM.

CCM KWA WAKA MOTO

Sumaye amtangazia vita Lowassa
• Mwenyewe asema wananchi wa Monduli ndiyo msuli wake

CCM KWA WAKA MOTO

 
Lowassa awatimulia vumbi Sitta, Membe
 
APANGA MAJESHI YA URAIS 2015, ASEMA MONDULI NDIYO MSULI WAKE WA KISIASA

Rufani Ya Lema Yatikisa Arusha


Video Rufaa ya Godbless Lema
 
Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema akiwahutubia wafuasi wake baada ya Jaji MKuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman kuahirisha kesi ya rufaa ya aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema.Picha Zote na Jackson Odoyo Mussa Juma, Arusha MAWAKILI wanaomtetea aliyekuwa Mbunge wa Arusha, Godbless Lema wamedai mbele ya Mahakama Kuu Kanda ya Arusha kuwa mteja wao yuko huru kwa kuwa mahakama haikutengua ubunge wake.Katika kesi hiyo, Jaji Mkuu, Mohamed Othman Chande anawaongoza wenzake wa Mahakama ya Rufani, Salum Massati na Natalia Kimaro kusikiliza maombi ya rufani hiyo, inayopinga Lema kuvuliwa ubunge.

Mawakili hao wa Lema jana walitoa hoja ya kupinga hukumu hiyo kufuatia mabishano baina yao na upande wa utetezi kwa maelezo kuwa taratibu za ufunguaji wa rufaa hiyo zimekosewa. Awali wakili Alute Mughwai aliiomba mahakama hiyo kutupilia mbali rufani hiyo kwa kile alichoeleza kuwa ina upungufu mwingi wa kisheria na kikanuni. Wakili huyo alitaja baadhi ya kasoro za rufani hiyo kuwa ni hati ya kukaza hukumu (tuzo) ambayo imewasilishwa mahakamani hapo kutokuwa na mhuri wa Jaji Gabriel Rwakibarila aliyetoa hukumu ya kesi hiyo.
Alidai kuwa katika rufani hiyo pia kuna upungufu kuhusu tarehe za kuwasilishwa kwa rufani, pia baadhi ya vifungu vimekosewa.Wakili Mughwai alitoa kumbukumbu ya kesi kadhaa ambazo mahakama ya rufani ilizitupa baada ya kukosa hadhi ya kisheria kusikilizwa.

“Mawakili wa Lema walipaswa kabla ya kuwasilisha mahakamani rufani yao, kujiridhisha kama kuna upungufu katika nyaraka ambazo wanawasilisha mahakamani.”Alisema kubwa katika makosa ambayo amebaini katika rufani hiyo ni kuwasilishwa bila kuwekwa mhuri hati ya kukaza hukumu (tuzo) iliyotolewa na Jaji aliyetoa hukumu katika kesi ya awali.“Hapa nani ambaye anajua sahihi ya Jaji? Alihoji. Hawa mawakili walipaswa kushinikiza kuwekwa mhuri wa mahakama katika hukumu hiyo ili kuthibitisha uhalali wake,” alisema Alute. Hata hiyo, wakili huyo alisema badala yake, mawakili hao waliwasilisha mahakamani rufani hiyo ndani ya siku 29 tu baada ya hukumu, badala ya siku 60 ambazo walipewa.

Kwa kuwasilisha mahakama ya rufani, hukumu ambayo bado haina mhuri wa Jaji ni ukiukwaji wa kanuni na taratibu za mahakama.”Mughwai alidai kuwa katika mazingira ya sasa hakuna cha kurekebishwa katika rufani hiyo, badala yake itupwe na kuwataka wakata rufani kulipa gharama zote za kesi. Hata hivyo, hoja hizo zilipingwa na mawakili wa Lema ambao ni Tundu Lissu na Method Kimomogoro, ambao walidai kuwa hawakuwa na mamlaka ya kumlazimisha Jaji Rwakibarila kuweka mhuri.

Lissu alidai "Kama inaonekana sasa kuwa ni batili, basi hata uamuzi wa kumvua ubunge Lema ni batili," alisema. Wakili Kimomogoro Kwa upande wake, Wakili Kimomogoro alisema kisheria kasoro hizo ya mhuri wa mahakama na tarehe, haziwezi kusababisha rufani hiyo kutupwa kwani haziathiri madai ya msingi katika rufani.

Alidai kesi hiyo ya Lema ilikuwa ya kipekee kwani mara tu baada ya hukumu kutolewa faili lilipelekwa jijini Dar es Salaam na maombi ya nyaraka kadhaa za kesi hiyo yalitumwa kutoka Dar es Salaam.“Katika mazingira kama haya hatuwezi kuepuka makosa ya kibinadamu ambayo yanatambulika kisheria,” alidai Kimomogoro. Aliongeza kuwa katika hoja hiyo, waliandika kifugu namba 114 badala ya 113 kimakosa ya kiuchapaji, lakini hakipotoshi kitu chochote kwani kifungu hicho hakipo. Wakili Kimomogoro alisema wakili mwenzake, Mughwai ameshindwa kuzungumzia uamuzi ya kesi ambazo, hazikufutwa kutokana na kuwa na upungufu mdogo wa aina hiyo ambao kimsingi hauathiri rufani. Hata hivyo, alisema kama wakili huyo alibaini makosa hayo, katika uwasilishaji wa hoja zake, alipaswa pia kurekebisha kwa mujibu wa sheria ya mwaka 2009 ya mahakama. Kimomogoro pia aliwasilisha mahakamani hoja kadhaa za kisheria na uamuzi ya Mahakama ya Rufani za ndani na nje ya nchi, ambazo hazikutupilia mbali rufani ambazo zilikuwa na upungufu mdogo, kwani lengo la mahakama hizo ni kutafuta haki.
“Siyo kila kasoro au usumbufu kwenye hukumu unaweza kusababisha kutupwa rufani kwani kasoro zote zilizotajwa ni za makosa na uchapaji na nyingine ni za kiutaratibu tu,” alisema. Alifafanua kuwa makosa ambayo yanaweza kusababisha rufani kutupwa ni kama aina namba ya kesi, majina na wadhifa wa wadau katika shauri husika, mambo yanayolalamikiwa na mahakama imeamua nini.

Wakili huyo alifafanua kuwa jambo la kukosekana mhuri wa mahakama wa Jaji siyo kubwa na kusababisha kutupwa rufani kwani hakuna ambaye anapinga hukumu iliyowasilishwa mahakamani. Kwa upande wake, Wakili Mwandamizi wa Serikali, Vitalis Timoth alisema anaunga mkono hoja za mawakili wa Lema, kuwa pingamizi ya wakili Mughwai haina msingi wa kisheria.

Alisema hati ya kukaza hukumu (Tuzo) inatolewa chini ya sheria ya mwenendo wa makosa ya jinai na siyo chini ya sheria ya masijala za mahakama. Alisema siyo kazi ya jaji aliyetoa hukumu, kuweka mhuri hukumu yake bali hiyo ni kazi ya msajili wa mahakama na masijala za mahakama.

Kama hati ya kukaza hukumu ina matatizo anayepaswa kulaumiwa siyo mawakili bali ni mahakama ambayo ndiyo ilikuwa na mamlaka ya kuweka mhuri,” alisema. Alidai kuwa pingamizi ya awali ya rufani inapaswa kuwa na sifa mbili, kwanza iwe na suala la kisheria na pili iendane na kesi ya msingi.“Katika hoja za wakili Mughwai ni wazi inathibitika pingamizi hili halina matakwa ya kisheria kwani hata kama ikipitwa siyo kuwa itazuia kurejeshwa tena na kusikilizwa kwa rufani ya msingi.”Alidai ni busara kuacha kuwa na pingamizi ambazo zinaongeza gharama za kesi na muda wa kusikiliza.

Ushauri wangu kila shauri liamuliwe kwa mazingira yake na uamuzi wa sasa uzingatie mahakama katika kutenda haki,” aliongeza. Alidai kwamba kutupwa kwa hoja ya kutaka waomba rufani wachapwe mijeledi kwani kazi ya mahakama siyo kuchapa watu bali ni kutoa haki.“Tunashauri kusikilizwa rufani kwa kuzingatia sheria na ushahidi,” alisema. Jopo la Majaji Baada ya kutolewa kwa hoja za pande zote za mawakili, Jaji Chande na Jaji Massati waliwauliza maswali kadhaa mawakili hao na kujieleza na baadaye Jaji Chande alitangaza kuahirishwa kwa kesi hiyo hadi hapo itakapotangazwa. Jaji Chande alisema vikao vya Mahakama ya Rufani Kanda ya Arusha vimemalizika jana, hivyo uamuzi wa kutupwa kwa pingamizi la rufani hiyo au la utatolewa siku itakayopangwa na mahakama.

Baada ya uamuzi huo umati wa wafuasi wa Chadema, uliokuwa ndani na nje ya mahakama ulianza kuimba nyimbo mbalimbali kama vile Lema Jembe na bila Lema patachimbika. Katika hatua ya kuepuka vurugu, Lema alizungumza na wafuasi hao nje ya mahakama na kuwataka kuondoka kwa amani kwenda katika ofisi ya Chadema iliyopo Ngarenaro kwa amani bila vurugu.

Warufaniwa katika kesi hiyo ni makada wa CCM, Happy Kivuyo, Mussa Mkanga na Agnes Mollel ambao walishinda kesi ambayo hukumu yake ilimvua ubunge Lema Aprili 4, mwaka huu.


 Chanzo: http://www.mwananchi.co.tz/habari

Tuesday 2 October 2012

VIONGOZI WA BAVICHA TAIFA WAALIKWA KUHUDHURIA MKUTANO MKUU WA BARAZA LA VIJANA LA CHAMA TAWALA NCHINI UJERUMANI


Mwenyekiti wa BAVICHA Taifa John Heche na Katibu Mkuu wake Deogratius Munishi wamealikwa na Baraza la vijana la chama tawala nchini Ujerumani kuhudhuria mkutano wake mkuu.
Vijana hao wa BAVICHA wamealikwa kama wawakilishi kutoka Tanzania na Africa kwa ujumla.Pia wamepewa heshima kubwa ya kuhutubia mkutano huo mkuu.
Mkutano mkuu huo utahudhuriwa na Chancellor wa Ujerumani Bi. Angel Markel.

RUFAA YA MH. GODBLESS LEMA YAAHIRISHWA Yapigwa ‘Kalenda’

 
Kwa mwendelezo wa jinsi kesi iliyokuwa mahakamani na maoni ya watanzania mbalimbali tembelea:  http://www.jamiiforums.com/jukwaa-la-siasa/331912-live-updates-mwendelezo-wa-kusikilizwa-rufaa-ya-lema-oktoba-02-2012-a.html

M4C yazoa makada 201 wa CCM kwa Dk. Magufuli

 
Mikutano ya Vuguvugu la Mabadiliko (M4C) inayofanywa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) wilayani hapa, Mkoa wa Geita, imezoa makada 201wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), akiwamo Mwenyekiti wa
Kitongoji cha Buhungu, Kata ya Kigongo.

Makada waliotimkia Chadema kutoka Jimbo la Chato linalowakilishwa na Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, kwa nyakati tofauti, wanatoka katika Kijiji cha Muganza, Kasenga, Busaka na Igando, Kata ya Bwera, ambako chama hicho kimefanya mikutano ya hadhara.

WanaCCM hao walidai wamekihama chama hicho kwa sababu wamechoshwa na mwenendo wa siasa zake, walizodai zimechangia maisha ya wananchi kuwa magumu.
CHANZO: NIPASHE

Mbunge awachochea wananchi Karatu

 
MBUNGE wa Karatu, Mchungaji Israeli Natse (CHADEMA), amewahamasisha wananchi wake wa Kata ya Baaray, Tarafa ya Eyasi kuwacharaza viboko watendaji wa vijiji na kata kutokana na tuhuma za kuchukua rushwa na kuruhusu wafanyabiashara wa vitunguu kukata miti na kulima katika chanzo cha maji cha Qangded.
Mchungaji Natse alitoa kauli hiyo juzi wakati akihutubia wananchi katika Kijiji cha Jobaj ambacho ni miongoni mwa vijiji saba vinavyotegemea chanzo hicho cha maji.
Alisema uamuzi wa kuwacharaza viboko watendaji hao, unatokana na ulegelege unaoonyeshwa na Serikali ya Rais Jakaya Kikwete katika kusimamia sheria na kanuni za utumishi.
Mchungaji Natse yupo jimboni akiambatana na wabunge wengine na viongozi kadhaa wa CHADEMA kutembelea vijiji mbalimbali kuangalia sakata la uharibifu wa mazingira lililofanywa na wafanyabiashara katika bonde la Mto Eyasi.
Wabunge wengine alioambatana nao ni Kabwe Zitto (Kigoma Kaskazini), Rose Kamili (Viti Maalum), Tundu Lissu (Singida Mashariki), Pauline Gekul (Viti Maalum) na Joshua Nasari (Arumeru).
Akiwahutubia wananchi katika vijiji saba vinavyozunguka bonde hilo la Eyasi, Natse alisema uharibifu huo unachangiwa kwa kiasi kikubwa na udhaifu wa Serikali ya Rais Kikwete.
Natse alieleza kuwa uharibifu uliofanywa na wafanyabiashara watano katika vyanzo hivyo vya maji katika bonde la Ziwa Eyasi, ulianza kushughulikiwa vizuri na Mkuu wa Wilaya hiyo, Daudi Ntibenda kwa kuwakamata waharibifu hao, lakini maagizo ya kichama yaliyotolewa na kuongezwa shinikizo la Mkuu wa Mkoa wa Arusha, yalifanya watuhumiwa hao kuachiwa bila masharti.
Alisema hali hiyo inatokana na ulegelege wa Serikali ya Rais Kikwete ambapo watumishi wake wa ngazi za kati na chini wanajiamulia mambo bila kujali madhara ya uamuzi huo wanaoufanya kwa wananchi na hata kwa chama chao cha siasa wanachokitumikia.
“Naomba Kikwete anisikie na Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo. Ulegelege wa serikali hii ndio unaotaka kuhatarisha maisha ya wakazi wanaozunguka bonde hili kwa kuwalinda wafanyabiashara wa vitunguu waliofyeka miti katika vyanzo vya maji na wao kuweka mashine 32 za kuvutia maji kwenda kwenye mashamba yao kwa kuwa wanaifadhili CCM,” alisema Natse.
Alifafanua kuwa wanatoa muda wafanyabiashara hao waondoke wenyewe kabla harakati hazijaanza kwa kutumia wananchi kuwatoa hapo kwa kuwa hakutakua na woga wa mabomu ya machozi wala virungu vya polisi wakati wa kuwaondoa.
Watuhumiwa wanaotajwa kuhusika na kuharibu chanzo hicho kikuu cha maji ni katika Kata ya Mang’ola ambao walikamatwa na mkuu wa wilaya na kuwekwa rumande kabla ya kuagizwa kuwaachia huru ni Waziri Saidi, Christopher Msemo, Loema Gilong, Girigisi Gidobad, Mamoya Muhindi na Sudi Omary.
Naye Kamili akihutubia wakazi wa Kijiji cha Jobag, aliwahamasisha kutozubaa kwa kuwa wao ndio wataathirika wa uharibifu huo, hivyo akawataka akina mama na vijana kufunga vibwebwe na kuhamia katika vyanzo hivyo kuondoa mashine hizo na kulilinda eneo hilo kwa muda wote.
Tanzania Daima

Zitto, Lissu wang’aka Karatu

MBUNGE wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto na mwenzake wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (CHADEMA), wamewaonya viongozi na madiwani wa chama hicho wilayani Karatu kuwa hawatavumiliwa endapo watashindwa kutatua tatizo la maji wilayani humo.
Vigogo hao walitoa msimamo huo mwishoni mwa wiki iliyopita wakati wakiwahutubia wakazi wa mji wa Karatu wakiwa wameongozana na Mbunge wa jimbo hilo, Mchungaji Israel Natse, katika mkutano wa kuhamasisha maendeleo pamoja na ushiriki wa wananchi katika utoaji wa maoni ya Katiba mpya.
Zitto ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa CHADEMA Bara, alisema akiwa kama kiongozi wa chama pamoja na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani bungeni, Lissu, wametoa maagizo kwa viongozi wao wa wilaya chini ya Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Lazaro Maasai, kwenda kuzungumza na wananchi kwenye vijiji ambavyo mradi wa maji wa Kaviwasu unapita.
Alifafanua kuwa lengo la kwenda kuzungumza na wananchi hao ni kujua matatizo yaliyopo ambayo yanasababisha mradi huo kutotoa huduma kwa kiwango kilichokusudiwa na kuyapatia ufumbuzi mara moja ili watu waendelee kupata maji safi na ya kutosha.
“Naomba niwambie wazi kama hawatatekeleza maagizo haya tutawafukuza wote kwa kuwa hatutakubali kuona mradi huo wa maji ulioasisiwa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa, wakati akiwa mbunge wa jimbo hili unaharibiwa na watu wachache wenye tamaa ya fedha,’’ alisema.
Aliongeza kuwa wametembelea maeneo hayo na kukutana na malalamiko mengi juu ya viongozi kushindwa kusimamia vema majukumu yao na kuwataka wananchi wawaambie viongozi hao kuwa katika miradi ya maendeleo hakuna siasa na ikibidi wawawajibishe kama watashindwa kutekeleza majukumu yao.
Akizungumzia kuhusu utoroshwaji wa fedha nje ya nchi unaofanywa na baadhi ya watendaji wa serikali, Zitto alisema tayari wana orodha ya Watanzania 27 ambao wanamiliki mamilioni ya dola nje ya nchi ambayo waliyapata kwa njia zinazotia shaka.
Zitto alitaja kuwa miongoni watuhumiwa hao yumo ofisa mmoja wa jeshi mstaafu ambaye hata hivyo hakumtaja jina, akisema anamiliki akaunti nje ya nchi ikiwa na kiasi cha dola milioni 56.
Aliitaka serikali iwataje wote wanaomiliki fedha nje na kuchukua hatua haraka, vinginevyo wao watawaweka hadharani kwa umma ili nguvu ya wananchi ichukue mkondo.
Naye Lissu akizungumza katika mkutano huo, aliwaonya wananchi wa Karatu wasikubali kuanza kurubuniwa kwa kuchukua visenti vidogo vidogo na kuharibu historia yao nzuri ya mfano kwa nchi hii.
Alisema vitendo vya kuendekeza njaa katika masuala ya utendaji si desturi na mfumo wa chama hicho, hivyo kuwatahadharisha wananchi kuwa kama kunatokea kiongozi ama mwanachama ana matatizo hayo basi hakuna kufichaficha waelezane hadharani.
Kuhusu utoaji maoni kwenye tume ya Katiba, Lissu aliwaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kama wanavyojitokeza kwenye mikutano ya chama hicho ili kutoa maoni yao.
“Naomba niwaambie wananchi nyie mna historia kubwa toka nchi inapata uhuru mliishawahi kuchagua kiongozi bila kupitia chama chochote, Chifu Sarwatt na mkambwaga mgombea wa TANU lakini leo miaka 50 ya uhuru tunaambiwa bado hatujakomaa kuwa na wagombea binafsi, kwa kutumia uandikwaji wa Katiba mpya jitokezeni mtoe maoni yenu,” alisema Lisu.
Alifafanua kuwa wasipojitokeza kutoa maoni kwa tume hiyo watakuwa wamechangia kuruhusu watu wachache kuwaandikia Katiba ama vipengele vingi vya Katiba ya zamani inayolalamikiwa vitabaki vilevile.
Tanzania Daima

KATUNI


WATOTO WA WASIRA WATOA UFAFANUZI JUU YA WAO KUJIUNGA NA CHADEMA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI UFAFANUZI KUHUSU SISI KUJIUNGA NA CHADEMA NA MALUMBANO KUHUSU MAJINA YETU


Tarehe 30/09/2012 mimi Esther Wasira na dada yangu Lilian Wasira tulijiunga na CHADEMA na kukabidhiwa kadi na Katibu Mkuu wa CHADEMA Mh. Dr Willibrod Slaa. Tulielezea kwa kirefu sababu za sisi kujiunga CHADEMA na tukasisitiza kuwa tumeridhika kuwa CHADEMA ni chama chenye dhamira safi ya kuiongoza Tanzania na kwamba ni chama kinacholeta matumaini mapya ya kuijenga Tanzania mpya yenye neema. Waandishi wa habari walijaribu sana kutudodosa kujua tuna uhusiano gani na Waziri Steven Wasira. Tulielezea wazi kuwa mahusiano yetu ya kifamilia hayahusiki na sababu na dhamira yetu ya kujiunga CHADEMA. Hata hivyo tulielezea kuwa Waziri Steven Wasira ni baba yetu mdogo ambaye alinyang'anyana ziwa na baba yetu mzazi, wakili George Wasira. Tulidhani hiyo ilitosha na lisingekuwa swala tena la kujadili na badala yake hoja ya kujadiliwa ingeweza kuwa sababu tulizozieleza za kujiunga CHADEMA. Tunasikitishwa sana na malumbano yaliyofuata baada ya hapo kuhusu kama sisi ni watoto wa Wasira au la. Kama tulivyoeleza, tumejiunga CHADEMA kwa sababu tulizozieleza hapo awali na wala si kwa sababu nyingine yeyote. Hatujajiunga CHADEMA kumdhalilisha mtu, kumfedhehesha mtu au kukipatia umaarufu CHADEMA kwa vile tu tunatumia jina la Wasira. CHADEMA ni chama cha siasa tena chenye wanachama na wafuasi wengi Tanzania hivyo si kashfa bali ni fahari kubwa mtu kujiunga CHADEMA na tena ni ushahidi wa mtu kujitambua. Pia CHADEMA ni Chama maarufu sana Tanzania kwa sasa hata pengine ni maarufu kuliko CCM hivyo hakihitaji kujipatia umaarufu kwa mgongo wetu. Sisi tunawaheshimu sana wazee wetu na tutaendelea kuwaheshimu ila linapokuja swala la chama cha kujiunga linabaki kuwa hiari yetu kwa kuzingatia sera za chama na uwezo wa chama husika katika kujenga Tanzania tunayoitaka na hilo ndilo lililotupeleka CHADEMA. Na hii ni haki yetu ya msingi kabisa inayolindwa na Katiba ya nchi hii chini ya ibara ya 20(1). Ikumbukwe kuwa mmoja wa Waanzilishi wa CHADEMA ni Mzee Wasira. Dhamira ya kuanzisha CHADEMA ilikuwa ni kushika dola na hili ndilo CHADEMA imekuwa siku zote inajaribu kuwashawishi Watanzania kuwa sasa wamekomaa na wanastahili kuchukua dola. Kwa vile kuchukua dola ilikuwa ndio ndoto ya baba yetu mzazi Mwanzilishi wa CHADEMA, sisi kama watoto tumejiunga na M4C ya CHADEMA ili tuweze kutimiza ndoto ya baba yetu kuwa CHADEMA siku moja ichukue jukumu la kuiongoza Tanzania.

Kwa maelezo zaidi wasiliana na:   
Lilian Wasira 0719 604156   
Esther Wasira 0655 048797

Chadema UK Ndani ya Milton Keynes

DAR NI SISI - VIDEO MAISHA YA WANADAR HATA BAADA YA MIAKA50 YA UHURU